Ticker

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

TANGAZO LA MSIBA NEW JERSEY-USA

TAFADHALI SAIDIA  KUTO ATAAEIFA KAMA UNAWAJUA NDUGU WA MAREHEMU


Tunaomba mtupostie tangazo hili katika blog zenu kama blog yako ni ya habari mbalimbali. Kuna kijana amefariki New Jersey, USA. Kijana aliyefariki alinajulikana kwa jina la Adolf, Brian au Tadeous Rwekagende. Alikua anasema alisoma Tambaza na alikua na mdogo wake anaitwa Rodrick Rwekagende ambaye naye alikua anaishi Texas. Ila cha kusikitisha ni kuwa huyo mdogo wake alisema alifariki mwaka jana mwezi wa nne (Tanzania).

Adolf alikua anasema baba yake na mama yake walifariki yeye na mdogo wake huyo wakiwa wadogo. Sasa yeye alikulia kwa mjomba wake. Juzi Adolf alipata massive stroke na kulazwa st Barnabas hospital, Livingston, NJ na kufariki. Mpaka sasa hivi kuna watu wametafuta ndugu zake na kumpata mjomba wake mmoja huko Bukoba vijijini. Hatukuweza kupata ndugu wa karibu hapa marekani na mpaka sasa hivi maiti yake ipo hospital haijawa claimed. Hivyo kama binadamu tumeamua kujichangisha ili tuweze kupeleka mwili wa mwezetu Tanzania kwa mazishi. Gharama za kuzika huku na kusafirisha kupeleka Tanzania ni karibu sawasawa tu hivyo tunaona ni bora akapumzike na ndugu zake Tanzania.

Hivyo tunaomba mtupostie kwenye blog zenu hili tangazo liwafikie watanzania watakaopenda kumsaidia ili apelekwe Tanzania tutashukuru sana. Tumefungua mahali pa kuchangisha helahttp://www.donationto.com/adolfsendhomecost au kama mtu anatumia paypal account ni adolffuneralcost@gmail.com. Tutawapa majina ya watu watakaokua kwenye kamati ya kukusanya hela mara tutakapomaliza kikao tunachotegemea kufanyika Jumamosi. na hela zote zitaonyeshwa zilivyotumika kama zipo extra zitapelekwa huko kwa wajomba zake Bukoba.

Na kama kuna mtu ana picha yake basi mtutumie kwa sababu hakuna mtu aliye na picha yake. ID yake ipo hospital hawawezi kumpa mtu mpaka wakishajua nani anachukua mwili na mahali alipokua anaishi hawaruhusu mtu kuingia kwa sasa mpaka wakishajua mazishi ni wapi au ndugu wa karibu ni wapi. Hivyo hamna mtu ana picha yake..

Please sisi hapa tunajitahidi ili azikwe kama ubinadamu hivyo huu sio muda wa kuanza kuuliza maswali kwa nini hiki wala kile...Kwa vile hata sisi tuna maswali mengi na hakuna mtu mweye jibu....Tunachojua ni kuwa alipata massive stroke na amefariki na hakuna ndugu yake wa karibu huku marekani.

Tunatanguliza shukurani na pia kama blog yako hupost mambo ya habari tunaomba utusaidie kuforward hii email kwa watu wengine...Kuna wazee wako NY kama wakikukubali kushughulikia huu msiba tutawatangazia na kuwapa information mpya. Na hela zitakazopatikana zitahamishiwa kwenye fund yeyote watakayofungua kama wataamua kufungua mpya au wataamua kuendelea na hi hii. Tunachotaka ni kusafirisha kijana wa watu Tanzania kwa sababu sasa hivi hilo ndio lengo letu....na hakuna mtu yeyote aliyesema kitu chochote hivyo kama kikao kikifanyika basi tutawaeleza linaloendelea.

Nitajitahidi kuupdate kinachoendelea katika twitter handle yangu @swahilimom
Regards,
Pauline

Post a Comment

1 Comments

Anonymous said…
Mtafuteni Gedi Rweyemamu au kaela kamanga Houston