Ticker

6/recent/ticker-posts

Header Ads Widget

Responsive Advertisement

TANGAZO LA MSIBA


 
Jesca Emmanuel (12),


Mhe. Tuvako Manongi, Balozi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, kwa majonzi makubwa, anasikitika
kutangaza kifo cha Jesca Emmanuel (12), Mtoto wa Afisa mwenzetu Bw.
Emmanuel Swere Alfred na Bi Doto, kilichotokea ghafla siku ya Jumapili
18/11/2012 katika Hospitali ya Mt. Sinai, Queens, New York. Taratibu na
mipango ya kuusafirisha Mwili wa Marehemu Mtoto Jesca kwenda kijijini
Bumbombi- Shirati Tanzania kwa mazishi zinaendelea kwa usimamizi wa
Ubalozi na Familia ya Marehemu.
Taarifa zaidi zitatolewa na Ubalozi kuhusu siku, tarehe na mahali
tutakapomuaga mpendwa wetu Jesca Emmanuel.
Raha ya Milele Umpe Eee Bwana na Mwanga wa Milele Umuangazie
apumzike kwa amani. Amina
UBALOZI WA TANZANIA UMOJA WA MATAIFA
NEW YORK

Post a Comment

0 Comments